Numbers 15:37-41

37Bwana akamwambia Musa, 38 a“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo. 39 bMtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu. 40 cNdipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu. 41 dMimi Ndimi Bwana Mwenyezi Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mwenyezi Mungu wenu.’ ”
Copyright information for SwhKC